HALI YA ARIEL SHARON YAZIDI KUWA MBAYA - Arnold Kayanda
Thursday

Hali ya kiafya ya waziri mkuu wa zamani wa Israel, Ariel Sharon - ambaye amekuwa katika hali mahututi, inaendelea kuzorota zaidi


Inaarifiwa kwamba maisha yake yamo hatarini.
Madaktari wanasema kuwa Sharon mwenye umri wa miaka , 85, anakabiliwa na matatizo ya afya ya viungo vyake vya mwili ikiwemo Figo zake na kwamba vinaanza kuonekana kutofanya kazi vyema.
Hata hivyo madaktari hawakutoa taarifa zaidi kuhusu afya ya Sharon.