Hii ni habari nzuri kwa familia ya Shakira na mpenzi wake Gerard Pique Baada ya kujifungua Mtoto Kiume - Arnold Kayanda
Friday

Familia ya mwanasoka mahiri Gerard Pique na mkewe Shakira wamepata ugeni mpya ndani ya familia hiyo baada ya mwanamuziki huyo kujifungua mtoto wa pili wa kiume

Mtoto huyo aliyepewa jina la Sasha likiwa na maana ya Alexander kwa lugha ya Kirussia, alizaliwa katika hospitali iliyopo katika mji wa Barcelona usiku wa kuamkia leo kwa njia ya upasuaji.