Michuano
ya GoTv Senior Cecafa Challenge Cup imefikia mwisho wake hii leo kwa
mchezo wa fainali uliowakutanisha wenyeji The Harambee Stars ya Kenya na
timu ya taifa ya Sudan maarufu kwa jinal la Utani la The Falcons .
Katika mchezo huo Kenya ilifanikiwa kubakisha kombe hilo nyumbani kwa kuwafunga Sudan 2-0 .
Mabao yote mawili yalifungwa na mshambuliaji na nahodha wa timu hiyo Allan Wanga ambaye huchezea klabu ya Fc Leopards .
Kabla ya mchezo huo wa fainali kulikuwa na mchezo wa kuwania nafasi ya ushindi wa tatu ambapo Timu ya taifa ya TANZANIA BARA ilishika nafasi ya nne baada ya kufungwa na Zambia kwa mikwaju ya Penati .
Mchezo huo uliisha kwa sare ya 1-1 baada ya Zambia kufunga kupitia kwa Ronald Kampamba huku Tanzania ikisawazisha kupitia kwa Mbwana Samatta .
Katika Mikwaju ya penati , Mrisho Ngassa, Haruna Channongo na Kelvin Yondani walikosa penati zao na kuipa Zambia ushindi wa tatu . Fainali inayowakutanisha Sudan na Wenyeji Kenya itapigwa saa 12 jioni .
Hii ni mara ya kwanza kwa Kenya kutwaa ubingwa huo baada ya kuukosa kwa miaka 11 tangu walipotwaa mara ya mwisho mwaka 2002 wakiwafunga Tanzania Bara huko Mwanza kwa matokeo ya 3-2 .
Historia nyingine iliyowekwa na Harambee Stars ni ile ya kutwaa taji hilo kwenye ardhi ya nyumbani kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1983 ilipowafunga Zimbabwe 1-0
Mchezo huo uliisha kwa sare ya 1-1 baada ya Zambia kufunga kupitia kwa Ronald Kampamba huku Tanzania ikisawazisha kupitia kwa Mbwana Samatta .
Katika Mikwaju ya penati , Mrisho Ngassa, Haruna Channongo na Kelvin Yondani walikosa penati zao na kuipa Zambia ushindi wa tatu . Fainali inayowakutanisha Sudan na Wenyeji Kenya itapigwa saa 12 jioni .
Hii ni mara ya kwanza kwa Kenya kutwaa ubingwa huo baada ya kuukosa kwa miaka 11 tangu walipotwaa mara ya mwisho mwaka 2002 wakiwafunga Tanzania Bara huko Mwanza kwa matokeo ya 3-2 .
Historia nyingine iliyowekwa na Harambee Stars ni ile ya kutwaa taji hilo kwenye ardhi ya nyumbani kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1983 ilipowafunga Zimbabwe 1-0