
12 Year a Slave
Nyong’o alipata sifa kemkem kwa jinsi alivyocheza kama msichana mtumwa katika sinema hiyo ambayo ilikuwa inahusu Mmarekani mweusi aliyekuwa huru lakini akahadaiwa na kuuzwa katika utumwa. Wiki hii Nyong’o alikuwa mmoja wa wanawake waliong’ara katika tuzo za Golden Globe award huko Hollywood ambako sinema ya “12 Years a Slave” alijizolea tuzo mbali mbali.
Captain Phillips
Nyong’o atakumbukwa kwa uchezaji wake mzuri katika mfululizo wa tamthiliya ya MTV Shuga iliyofanyika Nairobi, Kenya, na kurushwa hewani mwaka 2009 katika nchi kadhaa za Afrika. Katika MTV Shuga Nyong’o na waigizaji wengine vijana wa Kenya waliigiza katika aina mbali mbali kuonyesha hatari za kuambukizana virusi vya HIV katika maisha ya kila siku ya vijana barani Afrika.