Miss South Africa Rolene Strauss ameibuka mrembo wa dunia wa mashindano ya Miss World 2014, akiwashinda zaidi ya warembo 120 katika shindano lililofanyika jijini London, Uingereza.

Washindi wa tano wa mwanzo katika mashindano ya urembo ya mwaka
huu walikuwa kutoka Uingereza, Marekani, Hungary, Australia na Afrika Kusini.
Shindano la Miss World 2014 pia lilikuwa na mshindano tanzu na
mataji mengi, ambayo yalifanyika kuelekea siku ya fainali kuu.
Kwa mara ya kwanza, washindani watano walitangazwa kuwa Warembo
wa Miss World 2014 wenye Lengo: Washindi hao ni Miss India, Miss Kenya, Miss
Brazil, Miss Indonesia and Miss Guyana.